Ezekiel 27:1-6
Maombolezo Kwa Ajili Ya Tiro
1Neno la Bwana likanijia kusema: 2 a“Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Tiro. 3 bUmwambie Tiro, ulioko kwenye lango la bahari, ufanyao biashara na mataifa mengi ya pwani, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “ ‘Ee Tiro, wewe umesema,“Mimi ni mkamilifu katika uzuri.”
4 cMipaka yako ilikuwa katika moyo wa bahari,
wajenzi wako walikamilisha uzuri wako.
5 dWalizifanya mbao zako zote
kwa misunobari itokayo Seniri; ▼
▼ Yaani Hermoni.
walichukua mierezi kutoka Lebanoni
kukutengenezea mlingoti.
6 fWalichukua mialoni toka Bashani
wakakutengenezea makasia yako;
kwa miti ya msanduku
kutoka pwani ya Kitimu
wakatengeneza sitaha ▼
▼ Yaani sakafu ya merikebu au mashua.
yakona kuipamba kwa pembe za ndovu.
Copyright information for
SwhKC